Vibrant

Wednesday 12 August 2015

Mwili wa aliyekuwa Mhasibu Mkuu wa Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. Boniphace Haule aliyefariki nchini India wawasili jijini Dar es Salaam

Mwili wa aliyekuwa Mhasibu Mkuu wa Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. Boniphace O. Haule ukiwa katika gari baada ya kupokelewa katika kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Mwalimu J.K Nyerere.

Baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma waliofika kuupokea Mwili wa aliyekuwa Mhasibu Mkuu wa Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. Boniphace O. Haule ulipowasili katika kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Mwalimu J.K Nyerere.

TANZIA





Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. HAB Mkwizu anasikitika kutangaza kifo cha Bw. Boniphace Haule - Mhasibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma (Pichani) kilichotokea nchini India tarehe 10.08.2015.
Mwili wa Marehemu utawasili leo, uwanja wa ndege wa J.K. Nyerere. Mazishi yatafanyika Ijumaa tarehe 14/08/2015. Msiba uko nyumbani kwa marehemu Tegeta Ununio, Mtaa wa Mwaitende.

Maziko yanatarajia kufanyika katika makaburi ya KINONDONI.

Taarifa na taratibu za msiba zitafuata.

Monday 13 July 2015

MKUTANO WA 12 WA WAKUU WA UTUMISHI WA UMMA WA JUMUIYA YA MADOLA BARANI AFRIKA WAANZA


Mmoja wa Wajumbe wa mkutano wa Wakuu wa Utumishi wa Jumuiya ya Madola Barani Afrika kutoka Afrika Kusini Bi.Colette Clark akipokewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni  Y. Sefue katika Kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam leo.

Taswira ya moja ya eneo mkutano wa Wakuu wa Utumishi Barani Afrika utakapofanyika.


Mmoja wa Wajumbe wa mkutano wa Wakuu wa Utumishi wa Jumuiya ya Madola Barani Afrika kutoka Sierra Leone Bw. Ernest Surrur (kushoto) akipokewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni  Y. Sefue katika Kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam leo.


Mmoja wa Wajumbe wa mkutano wa Wakuu wa Utumishi wa Jumuiya ya Madola Barani Afrika kutoka Rwanda Bw. Gaspard Musonera akipokewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni  Y. Sefue katika Kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam leo.

Sunday 12 July 2015

MKUTANO WA 12 WA WAKUU WA UTUMISHI WA UMMA WA NCHI ZA AFRIKA WANACHAMA WA JUMUIYA YA MADOLA KUFUNGULIWA LEO na Mh. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Y. Sefue akiongoza kikao cha maandalizi ya Mkutano wa  kumi na mbili (12) wa Wakuu wa Utumishi wa Umma wa nchi za Afrika Wanachama wa Jumuiya ya Madola  utakaofunguliwa leo.

 Katibu Wakuu na watendaji mbalimbali wakijadili wakati wa kikao: kushoto ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu . Dkt. Florens Turuka, akifuatiwa na Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Menejimneti ya Utumishi wa Umma Bw. HAB Mkwizu na Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Adelhem James Meru.

 Taswira ya moja ya eneo mkutano wa Wakuu wa Utumishi Barani Afrika utakapofanyika.

Thursday 11 June 2015

6th Annual UNPAN Workshop in Johannesburg,South Africa

Executive Director of  the Center for Public Service Innovation (CPSI) Ms. Thuli Radebe giving welcoming remarks during the opening of 6th Annual Workshop held in Johannesburg, South Africa.

Session  in progress with delegates listening to UNDP Director for South Africa Mr. Walid Badawi.

Executive Director of the Center for Public Service Innovation (CPSI) Ms. Thuli Radebe offer a gift  to UNDP Director for South Africa Mr. Walid Badawi.


CPSI Programme Director   Mr. Pierre Choonraad moderate the event during day one at Emperors palace in Johannesburg.