Vibrant

Thursday 3 April 2014

TFDA YATOA MATOKEO YA UKAGUZI MAALUM WA MADUKA YA BIDHAA ZA VYAKULA JIJINI DAR, YAWATAKA WANANCHI KUJENGA UTARATIBU WA KUSOMA MAELEZO YA BIDHAA KABLA YA KUNUNUA.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA) Bw.Hiiti Sillo akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu ukaguzi maalum wa maduka ya kuuzia vyakula   “Supermarkets”
 na Mini-Supermarkets  katika jiji la Dar es salaam.

 Mkurugenzi wa Usalama na Chakula wa TFDA Bw. Raymond  Wigenge akitoa ufafanuzi kwa waandishi kuhusu hatua zinazochukuliwa na TFDA kuhakikisha usalama wa vyakula na Dawa nchini .TFDA imekuwa ikiongeza nguvu katika kukabiliana na bidhaa zisizokidhi viwango kwa kushirikiana na mamlaka nyingine za udhibiti kwa kukagua, kukamata na kuchukua hatua za kisheria ikiwemo kuwafikisha wanaokiuka sheria.

 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA) Bw.Hiiti Sillo (kulia) akitoa ufafanuzi wa baadhi ya bidhaa zilizokamatwa katika ukaguzi maalum kwenye maduka ya kuuzia vyakula   “Supermarkets” na Mini-Supermarkets  katika jiji la Dar es salaam zikiuzwa kinyume cha sheria ya Chakula , Dawa na Vipodozi sura ya 219. Wengine ni Mkurugenzi wa Usalama naChakula wa TFDA Bw. Raymond  Wigenge,na Meneja wa Ukaguzi wa Chakula wa TFDA kanda ya Mashariki Bw. Emmanuel Alphonce.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA) Bw.Hiiti Sillo (kulia) akitoa ufafanuzi wa maziwa yaliyokamatwa yakiwa kwenye kifungashio kisichokua na maelezo yoyote yakiuzwa kwenye maduka ya kuuzia vyakula   “Supermarkets”na Mini-Supermarkets  katika jiji laDar es salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA) Bw.Hiiti Sillo (kulia) akitoa ufafanuzi wa baadhi ya bidhaa zilizokamatwa katika ukaguzi maalum kwenye maduka ya kuuzia vyakula   “Supermarkets” na Mini-Supermarkets  katika  jiji la Dar es salaam zikiuzwa kinyume cha sheria ya Chakula , Dawa na Vipodozi sura ya 219. Wengine ni Mkurugenzi wa Usalama na Chakula wa TFDA Bw.Raymond  Wigenge, na Meneja wa Ukaguzi wa Chakula wa TFDA kanda ya Mashariki Bw. Emmanuel Alphonce.

 Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA)Bi. Gaudensia Simwanza akiwaonesha waandishi wa habari baadhi ya bidhaa zilizokamatwa na mamlaka hiyo  zikiwemo chumvi, vinywaji, maziwa ya watoto ambazo hazijasajiliwa na mamlaka hiyo kufuatia ukaguzi maalum uliofanyika katika jiji la Dar es salaam.

 Maziwaya watoto aina ya SMA 1,2 na 3, Promil Gold, S-26 Gold, Nursoy, Progress Gold, Cow &Gate, Isomil 2 na Infacare Soya , Nutrikids na Aptimil 1 yaliyokamatwa ambayo hayajasajiliwa na TFDA .


 Vinywaji baridi ambavyo havikusajiliwa na TFDA vilivyokamatwa kufuatia ukaguzi maalum katika jiji la Dar es salaam.Picha na 10.Bidhaa za chumvi ambazo hazikusajiliwa na TFDA zilizokamatwakufuatia ukaguzi maalum katika jiji la Dar es salaam.