Vibrant

Wednesday 26 March 2014

MH. WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA AWATAKA WAJUMBE BUNGE LA KATIBA KUEPUKA MIVUTANO




Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Kayanza Peter Pinda akiongea na waandishi wa habari leo mjini Dodoma juu ya mambo mbalimbali ikiwemo kuwaomba wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kuepuka mivutano na badala yake wazingatie mambo muhimu yatakayosaidia Taifa na Watanzania kupata Katiba mpya .

WAJUMBE BUNGE LA KATIBA WATAKIWA KUZINGATIA MASLAHI YA TAIFA

Na  Magreth  Kinabo – Maelezo, Dodoma
Baadhi ya wajumbe wa Bunge la Maalum la Katiba wamewataka wajumbe wenzao kujitika katika mchakato wa mjadala wa Rasimu ya Katiba Mpya  itakayozingatia maslahi ya taifa na kuwanufaisha Watanzania badala kujitazama mwenyewe.

Kauli hiyo imetolewa leo na mjumbe wa bunge hilo, ambaye ni mmoja wa kiongozi wa kundi la TANZANIA KWANZA Dk. Emmanuel Nchimbi  wakati akizungumza katika kipindi cha Jambo  kinachorushwa na Shirika la Utangazaji la  Tanzania(TBC), ambapo alisema msingi wa kundi hilo ni kushiriki katika mchakato huo  na kuaichaTanzania ikiwa moja.
“ Tunataka kushiriki katika kumaliza kazi ya  Bunge hili na kuaicha Tanzania ya leo na Kesho baada kumaliza ,” alisema Dk. Nchimbi.

 Aidha DK . Nchimbi alisema  kuwa mchakato huo usiwe sehemu ya kujipatia madaraka, bali iwe ya kuwaongoza Watanzania katika kuwapatia maendeleo.
Alisema bado watu wana mahitaji makubwa ya huduma za kijamii kama vile  elimu, afya, ufugaji, na miundombinu.

Dk. Nchimbi akifafanua kuhusu suala la kura ya wazi au siri, alisema bado msimamo wake  ni wa kura ya wazi  ambao utajenga mfumo wa maadili ya ukweli na uwazi, huku akihoji kama wanachangia mjadala kwa wazi kwa nini kura zisipigwe kwa wazi?
Alisema kura ya wazi itasaidia wananchi kutambua michango yao katika maeneo mbalimbali ilivyowakilishwa.

 “Tuko hapa kutunga Katiba ya Watanzania mtu atakumbukwa kwa kile alichokisema,” alisisitiza.

Kwa upande wake mjumbe mwingine wa  kundi hilo , Charles Mwijage akingumza katika kipindi hicho aliwataka wajumbe wa Bunge hilo kutumia njia ya maridhiano pale wanapoona kuna mambo ambayo hajaridhika nayo.

 Akizungumzia kuhusu suala la kuwepo kwa Serikali tatu alisema , lina gharama ya kuuendeshaji kwani ,italazimika kuwa na tume nane kuwa na mabunge matatu yenye viongozi tofauti ambayo yataongeza gharama

 Akizungumza baada ya kuahirishwa wa kikao cha  Bunge hilo, mjumbe kutoka Asasi ya Vijana, Siti Abbas Ali , ambaye pia ni Mwanasheria kutoka Chama cha Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) aliwataka Watanzania kuondoa hofu juu ya  mchakato huo,hivyo katiba hiyo itakuwa ni ya Watanzania.

 Alisema wataangalia kwa upana haki za vijana, watoto, wanawake na makundi maalum kwa upana. Mwisho.

TAMKO RASMI LA MTANDAO WA WATU WA PEMBA WAISHIO TANZANIA BARA

NEPPELTA
NETWORK FOR PEOPLE OF PEMBA LIVING IN TANZANIA MAINLAND
MTANDAO WA WATU WA PEMBA WAISHIO TANZANIA BARA

MAKUNGANYA STREET/ KARIAKOO
P.O. BOX 21243
DAR ES SALAAM
23/03/2014


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.
TAMKO RASMI LA KUUNGA MKONO HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MH. DK. JAKAYA MRISHO KIKWETE LIYOITOA KWA BUNGE MAALUMU LA KATIBA, DODOMA TAREHE 21/03/2014.

Ndugu,
          Waandishi wa habari, Tunamtanguliza Mwenyezi Mungu mwingi wa rehemu, heri na Baraka.
Mpango wa kuunganisha nchi za Zanzibar na Tanganyika ambao mchakato wake ulianza mwaka 1963 ulikuwa ni utashi wa Viongozi wetu wawili Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Marehemu Mzee Abeid Aman Karume.
Wote wawili kupitia vikao vyao mbalimbali walikubaliana kuziunganisha nchi hizi kwa maslahi mema ya wananchi wao. Hatua hiyo ilipewa Baraka na Mabunge ya nchi hizi mbili na miswada ya sheria ya kuunganishwa ilipitishwa na ikatungwa sheria iliyopelekea kufanyika tendo la Muungano wa Tanganyika na Zanzibar tarehe 24 Aprili 1964.
Dhima ya Muungano wetu pamoja na mambo mengine ni kuimarisha historia ya vizazi vya nchi hizi mbili ambazo zina asili zinazofanana na historia za asili hizi zilivurugwa na Wakoloni wa Kijerumani, Kiingereza na hatimaye utawala wa Sultan.
Tangu Muungano ufanyike kumekuwa na mabadiliko mbalimbali hasa katika mahusiani ya kibiashara.
Sisi Watanzania wenye asili ya Pemba tunaoishi huku Bara tumefaidika na tunaendelea kufaidika sana na uwepo wa Muungano. Ukiachilia suala la ajira za Serikalini, Muungano umesaidia kukua kwa biashara zetu ambapo mtaji wa Wapemba pekee wanaoishi huku umeweza kufikia shilingi Trilioni 1.2. Hiki si kiasi kidogo kwa nchi kama Tanzania inayopigania ukuaji wa uchumi kupitia mitaji ya uwekezaji hasa wa kizalendo.
Idadi ya Wapemba wanaoishi Bara imeendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka ambapo hadi mwaka 2012 inakadiriwa kwa kufikia laki 8.3. Faida nyingine pia ni sisi kuoa au kuolewa na wenzetu wa Bara hali iliyochangia kuongezeka kwa mahusiano ya kindugu. Pia Wapemba wamejihusisha zaidi na Kilimo na ufugaji na kuongeza tija zaidi katika sekta hizo.
Hivyo basi kuwepo kwa dalili zozote za kuvunjika kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar hakuwezi kutuacha salama sisi Wapemba tuishio huku Bara. Chokochoko zote na ishara mbaya za chuki kati ya Wabara na Wazanzibar hazitaweza kuimalisha msingi mkubwa wa Muungano uliojengwa kwa muda mrefu chimbuko lake likiwa ni waasisi wetu.
Kwa hatua hiyo basi mtandao wetu umeona si vyema kukaa kimya bila kumpongeza Rais wetu Dk. Jakaya Kikwete kwa hotuba nzuri iliyojaa hekima, busara, uzalendo na upole. Sisi tumefarijika sana Rais wetu kukemea Serikali tatu kwa kuonyesha udhaifu wa kila mmoja huku akijenga hoja zenye mshiko kuhusu athari za Serikali hizo kwa uwepo wa Muungano huu.

UTUMISHI YAJADILI MASUALA YA KIUTUMISHI KWA NJIA YA ELEKTRONIKI NA OFISI ZA MIKOA YA PWANI,LINDI NA MBEYA

Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi Rasilimaliwatu Bw. Emmanuel Mlay (picha ndogo kulia) akiwasilisha mada katika kikao kazi kilichoendeshwa kwa njia ya kielektroniki (video conference) kwa pamoja na mikoa ya Pwani, Mbeya na Lindi mapema leo