Vibrant

Wednesday 12 August 2015

Mwili wa aliyekuwa Mhasibu Mkuu wa Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. Boniphace Haule aliyefariki nchini India wawasili jijini Dar es Salaam

Mwili wa aliyekuwa Mhasibu Mkuu wa Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. Boniphace O. Haule ukiwa katika gari baada ya kupokelewa katika kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Mwalimu J.K Nyerere.

Baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma waliofika kuupokea Mwili wa aliyekuwa Mhasibu Mkuu wa Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. Boniphace O. Haule ulipowasili katika kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Mwalimu J.K Nyerere.

TANZIA





Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. HAB Mkwizu anasikitika kutangaza kifo cha Bw. Boniphace Haule - Mhasibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma (Pichani) kilichotokea nchini India tarehe 10.08.2015.
Mwili wa Marehemu utawasili leo, uwanja wa ndege wa J.K. Nyerere. Mazishi yatafanyika Ijumaa tarehe 14/08/2015. Msiba uko nyumbani kwa marehemu Tegeta Ununio, Mtaa wa Mwaitende.

Maziko yanatarajia kufanyika katika makaburi ya KINONDONI.

Taarifa na taratibu za msiba zitafuata.