Vibrant

Friday 25 April 2014

Lets just fight! Kansiime Anne

UTUMISHI YAICHAKAZA CDA MASHINDANO YA MEI MOSI

Na. James Katubuka
Timu ya Mpira wa pete ya ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma imeendelea kujiweka katika nafasi nzuri ya kuwa bingwa wa michuano ya Mei Mosi mwaka huu mara baada ya kuilaza CDA ya Dodoma magoli 42 dhidi 15 katika mchezo uliofanyika jana Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Mchezo huo ulikuwa na ushindani wa aina yake kutokana wachezaji wengi wa CDA kuwa ni wazoefu na Ofisi ya Rais Utumishi kuwa na wachezaji ambao wengi wao wameshaichezea timu ya Taifa kwa nyakati tofauti.

Licha ya washabiki wa mpira wa pete mjini Morogoro kushuhudia burudani safi pia walishuhudia jahazi la timu ya CDA likizama katika kipindi cha kwanza kwa kubugizwa  magori 16 dhidi ya matano katika mchezo huo.

Hadi mwamuzi wa mchezo huo anapuliza kipenga cha mwisho kuashiria mchezo huo kwisha, wachezaji wa Ofisi ya Rais Utumishi Fatuma Machenga (GA) na Mwadawa Twalibu (GS) walishirikiana vema kuilaza CDA mabao 42 dhidi ya 15.

Nao wachezaji Anna Msulwa (WA) na Elizabeth Fusi (C) walikuwa ni chachu ya ushindi kwa timu ya utumishi kutokana na kuwalisha vema Fatuma Machenga (GA) na Mwadawa Twalibu (GS) katika mchezo huo uliotawiliwa na ufundi na shamla shamla toka timu pande zote mbili.

Mara baada ya mchezo kumalizika, kocha wa timu ya CDA Dodoma Bi. Susan Nkurlu alisema kuwa mchezo ulikuwa mzuri na wa kuvutia hivyo aliwapongeza wachezaji wake na wa Utumishi kwa kutoa burudani safi kwa wapenzi wa mpira wa pete wa Morogoro.

“Kukosekana kwa kwa wachezaji wangu nyota wawili Goal Shooter (GS) na Wing Attack (WA) kumepelekea timu yangu kupoteza mchezo huu lakini naahidi kupata ushindi katika mechi ijayo dhidi ya TTPL” alisema Nkurlu.

Naye,Kocha wa timu ya Ofisi ya Rais (Utumishi) Bw. Mathew R. Kambona aliwapongeza wachezaji wake kwa kuibuka na ushindi mnono na kuhaidi kuyafanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza katika mchezo huo ili kutengeneza mazingira mazuri ya kuendeleza wimbi la ushindi katika  mechi ijayo.