Vibrant

Saturday 8 March 2014

Siku ya Wanawake Duniani ilivyofana jijini Dar es Salaam

Waziri wa TAMISEMI Mh.Hawa Ghasia akihutubia wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Mwembeyanga jijini Dar es salaam

Mkuu wa Mkoa wa Dar es  Salaam Bw. Said Meck Sadiq akihutubia wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika viwanja vya Mwembeyanga jijini Dar es Salaam 
Kikundi cha burudani cha Machozi Theatre kikitoa burudan kwenye maadhimisho hayo.

Baadhi ya watumishi wa Idara ya Uhamiaji wakiwa kwenye maandamano
Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma wakiwa tayari kwa kuanza maandamano kuelekea viwanja vya Mwembeyanga jijini Dar es Salaam
Waziri wa TAMISEMI Mh.Hawa Ghasia (kushoto) akiserebuka wakati wa maadhimisho ya Siku ya wanawake duniani kwenye viwanja vya Mwembeyanga jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Bw.Said Meck Sadick akimuunga mkono.
Baadhi ya washiriki kutoka ofisi mbalimbali za Serikali na binafsi wakitembelea mabanda kuangalia bidhaa wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wanawake duniani viwanja vya Mwembeyanga jijini Dar es Salaam.

Ofisi ya Rais-Utumishi yampongeza Balozi Mteule Dkt. Aziz Mlima

Katibu Mkuu Utumishi Bw.George D. Yambesi (katikati) akizungumza wakati wa hafla fupi ya kumpongeza Balozi mpya wa Tanzania nchini Malaysia Dkt. Aziz Mlima iliyofanyika ukumbi wa Utumishi hivi karibuni.Kushoto kwake ni Balozi Mteule Dkt.Aziz Mlima na kulia kwake ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Utawala na Utumishi Bi.Jane Kajiru.

Katibu Mkuu Utumishi Bw.George D. Yambesi (kushoto) akimkabidhi zawadi Balozi mpya wa Tanzania nchini Malaysia Dkt. Aziz Mlima katika hafla fupi ya kumpongeza iliyofanyika ukumbi wa Utumishi hivi karibuni. Kabla ya uteuzi huo Dkt. Aziz Mlima alikuwa  Msaidizi wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Benjamin William Mkapa.

Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya RaisMenejimenti ya Utumishi wa Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Utumishi Bw.George  Yambesi (hayupo pichani) wakati wa hafla ya kumuaga Balozi Mteule Dkt. Aziz Mlima iliyofanyika ukumbi wa Utumishi jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Balozi Mteule wa Tanzania nchini Malaysia Dkt. Aziz Mlima (wa pili kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma baada ya hafla fupi ya kumpongeza iliyofanyika ofisini hapo hivi karibuni.Kushoto kwake ni Katibu Mkuu Utumishi Bw.George Yambesi na Naibu Katibu Mkuu Utumishi Bw.HAB Mkwizu