Vibrant

Tuesday 8 April 2014

MWAKILISHI JIMBO LA KIEMBE SAMAKI ATIMIZA AHADI KWA TIMU ZA JIMBO LAKE

Mwakilishi wa Jimbo la Kiembe samaki Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (wakatikati) wakiteta jambo na Mwenyekiti wa CCM Jimbo la Kiembe samaki Ramadhan Mrisho wa kushoto, kulia Mwenyekiti wa Kamati ya michezo ya Jimbo hilo Juma Abdul-rabi kabla ya kukabidhi pesa taslim na vifaa vya michezo kwa tim za Jimbo hilo ikiwa ni ahadi aliyoitoa wakati wa kampeni zake hafla hiyo imefanyika katika Hoteli ya Ocean View Mjini Zanzibar.

Diwani wa Jimbo la Kiembe samaki Bw. Gharib Mohamed Addy akizungumza na wanamichezo wa Jimbo hilo (hawapo pichani)kabla yakukabidhiwa vifaa vya michezo na Mwakilishi wa Jimbo la Kiembe samaki Mhe. Mahmoud Thabit Kombo

Baadhi ya wanamichezo na viongozi mbalimbali wa Jimbo la Kiembe samaki wakimsikiliza Mwakilishi wa Jimbo hilo Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (hayupo pichani) kabla ya kukabidhi pesa na vifaa vya michezo kwa timu za Jimbo lake. 
Mhe. Mahmoud Thabit Kombo akimkabidhi pesa sh/= laki nne kiongozi wa tim ya Smoll Zico ya Kiembe samaki ikiwa ni ahadi aliyoito wakati wa kampeni zake.

(Picha na  Makame Mshenga,MAELEZO ZANZIBAR)

No comments: