Vibrant

Wednesday 30 April 2014

GOSSIP JOURNALIST GETS A SHOCK - Delivered From Demons!!!

MABADILIKO YA ANUANI YA OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA


Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma inapenda kuwafahamisha wadau wake kuwa anuani yake imebadilika hivyo kuanzia sasa mawasiliano yafanyike kwa kutumia anuani ifuatayo;

OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA
UTUMISHI HOUSE
8 BARABARA YA KIVUKONI
11404 DAR ES SALAAM
au
PRESIDENT’S OFFICE, PUBLIC SERVICE MANAGEMENT
UTUMISHI HOUSE
8 KIVUKONI ROAD
11404 DAR ES SALAAM

Anuani hii inachukua nafasi ya Sanduku la Posta 2483, Dar es salaam. Hivyo, mawasiliano yote yazingatie anuani mpya.

Limetolewa na
Katibu Mkuu
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma

Barua pepe; permsec@utumishi.go.tz

Tuesday 29 April 2014

UTUMISHI YATWAA UBINGWA MASHINDANO YA MEI MOSI 2014

Wachezaji wa Ofisi ya Rais, Utumishi wakipasha misuli moto (warm-up) jana kabla ya mechi ya mashindano ya Mei Mosi 2014 dhidi ya Uchukuzi iliyochezwa uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro
Mfungaji bora wa mshindano ya Mei Mosi 2014 wa mpira wa pete Fatuma Machenga (GS) wa Utumishi akiwa na kikombe cha ufungaji bora mara baada ya kukabidhiwa na mgeni rasmi wakati wa hafla fupi ya ufungaji wa mashindano hayo iliyofanyika jana Uwanja wa Jamhuri Morogoro.
Baadhi ya wachezaji wa Utumishi (jezi za kijani) wakishangilia ubingwa wa michuano ya Mei Mosi waliopata pamoja na baadhi ya wanamichezo wenzao toka taasisi mbali mbali mara baada mechi dhidi ya Uchukuzi iliyochezwa jana uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.


Mchezaji wa Uchukuzi (C) (mwenye mpira) akijianda kutoa pasi kwa huku  mchezaji wa Utumishi Sophia Komba akijianda kuunyaka mpira katika mechi ya mashindano ya Mei Mosi 2014 dhidi ya Uchukuzi iliyochezwa jana uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.


Na. James Katubuka
Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma imeibuka kinara wa mpira wa pete katika mashindano ya Mei Mosi ya mwaka huu yaliyofikia tamati jana katika kiwanja cha Jamhuri mjini Morogoro.

Utumishi walijikita kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo baada ya kuisambaratisha timu ya Wizara ya Uchukuzi kwa kuibugiza magoli 33 dhidi ya 21 katika mchezo uliokuwa na ushindani na msisimko wa aina yake uliorindima katika Uwanja mkongwe wa Jamhuri Morogoro.

Mchezaji Fatuma Machenga (GS) wa Ofisi ya Rais (Utumishi) alikuwa mwiba dhidi ya timu ya Uchukuzi kwa kuiongoza Utumishi vema katika mchezo huo.
Aidha,Goal Shooter (GS) huyo wa Utumishi ndiye mfungaji bora wa mashindano ya Mei Mosi kwa mpira wa pete ambapo amefunga magoli 136 yaliyopelekea kunyakua kikombe cha ufungaji bora.

Akizungumzia hali ya mchezo baada ya mwamuzi kupuliza kipenga cha mwisho, Mchezaji Subira Jumanne (WA) wa timu ya Uchukuzi alisema kuwa mchezo ulikuwa na ushindani mkubwa kwani walikutana na timu nzuri na iliyojiandaa vema.
“Asiyekubali kushindwa si mshindani hivyo tutafanya maandalizi ya kutosha ili katika mashindano yajayo nasi tuwe mabingwa” alisema Subira.

Naye,mfungaji bora wa mshindano hayo mchezaji Fatuma Machenga (GS) wa Utumishi akiwa mwenye furaha alisema kuwa anajisikia fahari kuiwezesha timu yake kuwa bingwa.

“Tutahakikisha kuwa mwakani tunapambana kwa hali na mali ili tuweze kutetea ubingwa wetu” alisema Machenga.

Utumishi imenyakua kombe hilo lililokuwa likishikiliwa na timu ya Wizara ya Ulinzi ambao ndio walikuwa mabingwa wa Mei Mosi 2013.Kikombe cha mshindi wa pili  kwa mwaka huu kimenyakuliwa na Wizara ya Mambo ya Ndani na mshindi wa tatu ni Wizara ya Uchukuzi.


Monday 28 April 2014

VACANCY ANNOUNCEMENT-AFRICAN RISK CAPACITY

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
PRESIDENT'S OFFICE
 


          Applications are hereby invited from qualified and experienced Tanzanians for the following Vacant post advertised by the African Risk Capacity (ARC)

·        Post :                            Director General
·        Duty Station :                Pretoria - South Africa
·        Deadline for Applications :  30th April 2014

SUBMISSION OF APPLICATIONS

For more information regarding Terms of Reference of the advertised posts; qualifications, tenure of appointment, and remuneration please visit the African Risk Capacity (ARC): http://www.africanriskcapacity.org/arcdg/application  

·        All the applications should be made through the online system only via the following website: erica.hovanibue@africanriskcapacity.org

·        Copy of the applications should be sent to the following address:-
                               
Permanent Secretary,
President’s Office-Public Service Management,
P.O. Box 2483,
DAR ES SALAAM.








Kansiime Anne ready to take on husband number 2

Sunday 27 April 2014

JIPATIE KITENGE ORIGINAL KUTOKA CONGO!


Sale!Sale!Sale!
Vitenge vya Wax Original kabisa kutoka nchini Congo.
Bei ni nafuu.Vimebaki vichache wahi chako sasa.
Kama unahitaji wasiliana nami kwa namba hii 0717080903

UTUMISHI YAENDELEA KUTOA VICHAPO MASHINDANO YA MEI MOSI MOROGORO

Mchezaji wa Ofisi ya Rais, Utumishi Lilian Sylidion (GK) akinyaka mpira na kuwazidi wachezaji wa CDA Dodoma  katika mechi iliyochezwa jana ya mashindano ya Mei Mosi 2014 katika  Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Mchezaji wa CDA ya Dodoma (mwenye mpira) akijianda kutoa pasi kwa huku akiwa kazingirwa na wachezaji wa Utumishi katika mechi iliyochezwa jana katika mashindano ya Mei Mosi 2014 yanayoendelea katika  Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Mwadawa Twalibu (GA) wa timu ya Ofisi ya Rais Utumishi akijiandaa kuchukua mpira licha ya upinzani wa wachezaji wa CDA Dodoma katika   mashindano ya Mei Mosi 2014 yanayoendelea katika  Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Mchezaji wa Ofisi ya Rais, Utumishi Sophia Komba  (C) akijiandaa kutoa pasi kwa Fatuma Machenga (GS) katika eneo la goli la wapinzani wao CDA Dodoma katika  mashindano ya Mei Mosi 2014 yanayoendelea katika  Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Friday 25 April 2014

Lets just fight! Kansiime Anne

UTUMISHI YAICHAKAZA CDA MASHINDANO YA MEI MOSI

Na. James Katubuka
Timu ya Mpira wa pete ya ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma imeendelea kujiweka katika nafasi nzuri ya kuwa bingwa wa michuano ya Mei Mosi mwaka huu mara baada ya kuilaza CDA ya Dodoma magoli 42 dhidi 15 katika mchezo uliofanyika jana Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Mchezo huo ulikuwa na ushindani wa aina yake kutokana wachezaji wengi wa CDA kuwa ni wazoefu na Ofisi ya Rais Utumishi kuwa na wachezaji ambao wengi wao wameshaichezea timu ya Taifa kwa nyakati tofauti.

Licha ya washabiki wa mpira wa pete mjini Morogoro kushuhudia burudani safi pia walishuhudia jahazi la timu ya CDA likizama katika kipindi cha kwanza kwa kubugizwa  magori 16 dhidi ya matano katika mchezo huo.

Hadi mwamuzi wa mchezo huo anapuliza kipenga cha mwisho kuashiria mchezo huo kwisha, wachezaji wa Ofisi ya Rais Utumishi Fatuma Machenga (GA) na Mwadawa Twalibu (GS) walishirikiana vema kuilaza CDA mabao 42 dhidi ya 15.

Nao wachezaji Anna Msulwa (WA) na Elizabeth Fusi (C) walikuwa ni chachu ya ushindi kwa timu ya utumishi kutokana na kuwalisha vema Fatuma Machenga (GA) na Mwadawa Twalibu (GS) katika mchezo huo uliotawiliwa na ufundi na shamla shamla toka timu pande zote mbili.

Mara baada ya mchezo kumalizika, kocha wa timu ya CDA Dodoma Bi. Susan Nkurlu alisema kuwa mchezo ulikuwa mzuri na wa kuvutia hivyo aliwapongeza wachezaji wake na wa Utumishi kwa kutoa burudani safi kwa wapenzi wa mpira wa pete wa Morogoro.

“Kukosekana kwa kwa wachezaji wangu nyota wawili Goal Shooter (GS) na Wing Attack (WA) kumepelekea timu yangu kupoteza mchezo huu lakini naahidi kupata ushindi katika mechi ijayo dhidi ya TTPL” alisema Nkurlu.

Naye,Kocha wa timu ya Ofisi ya Rais (Utumishi) Bw. Mathew R. Kambona aliwapongeza wachezaji wake kwa kuibuka na ushindi mnono na kuhaidi kuyafanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza katika mchezo huo ili kutengeneza mazingira mazuri ya kuendeleza wimbi la ushindi katika  mechi ijayo.






Wednesday 23 April 2014

MEMBE KUWA MGENI RASMI MKUTANO WA KIMATAIFA WA UALBINO

Na Frank Mvungi- Maelezo
WAZIRI wa wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe  anatarajiwa kuwa mgeni rasmi mkutano wa Kimataifa wa Ualbino utakaofanyika mwezi Mei mwaka huu.

Hayo yamesemwa na Afisa Mahusiano na habari wa Chama cha Albino Tanzania (TAS),  Josephat Torner wakati wa mkutano na waandishi wa Habari leo jijini Dar es salaam.

Torner alisema mkutano huo wa siku moja utafanyika katika hoteli ya Serena Jijini Dar es salaam na utawahusisha washiriki toka mataifa mbalimbali yakiwemo Nchi za Afrika Mashariki, Marekani, Nchi za Ulaya na Nchi za Kusini mwa Afrika.

Alisema moja ya matarajio ya mkutano huo ni kupata sauti ya pana ya Kimataifa kuutaka Umoja wa Mataifa kuitangaza tarehe 4 mwezi Mei kuwa Siku ya Kimataifa ya Ualbino.

Aliongeza kuwa lengo la maadhimisho ya siku hiyo ni kutafakari vikwazo vinavyosababisha tofauti ya umri wa kuishi kati ya watu wenye ulemavu na watu wengine.

“Hii inatokana na ukweli kwamba kwa Tanzania wastani wa umri wa kuishi kwa watu wenye ualibino ni miaka 30 wakati kwa watu wengine ni miaka 60”2, alisema Torner.

Alisema sababu zinazochangia watu wenye ulemavu wa ualbino kuishi nusu ya umri wa Watanzania wengine ni kukabiliwa na saratani ya ngozi.

Alitoa wito kwa watu wote wenye ualbino,wazazi,walezi na wadau mbalimbali na umma kwa ujumla kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho haya.

Maadhimisho ya Siku ya Albino yalianzishwa hapa nchini mwaka 2006 na tangu mwaka huo yamekuwa  yakileta hamasa katika nchi mbalimbali Duniani.

Kilele cha maadhimisho hayo hapa nchini kinatarajiwa kuwa siku ya tarehe  4/5/2014 na kauli mbiu ikiwa ni Haki ya Afya,Haki ya Uhai.



Wednesday 16 April 2014

SERIKALI YASAINI MKATABA WA KUSIMIKA MTANDAO WA MAWASILIANO WA SERIKALI

Katibu Mkuu Utumishi Bw. George D. Yambesi (katikati) akizungumza wakati wa hafla fupi ya kusaini mkataba wa kuweka Mtandao wa Mawasiliano wa Serikali  na kampuni za mawasiliano za SOFTNET Technologies na TTCL iliyofanyika ofisini kwake jana. Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Serikali ya Serikali Mtandao (eGA) Dkt Kuwe Bakari, kushoto ni Bw. Priscus Kiwango Mkurugenzi wa TEHAMA Utumishi, akifuatiwa na Mkurugenzi wa kampuni ya SOFTNET Ltd  Bw.Gilbert Herman 

Katibu Mkuu Utumishi Bw.George D. Yambesi (kushoto) akimkabidhi mkataba wa kuweka mtandao wa Mawasiliano wa Serikali Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Serikali Mtandao (eGA) Dkt.Kuwe Bakari wakati wa hafla fupi iliyofanyika ofisini kwake jana. 

Katibu Mkuu Utumishi Bw.George D. Yambesi akimkabidhi mkataba wa kuweka mtandao wa Mawasiliano wa Serikali Mkurugenzi wa kampuni ya  SOFTNET Technologies Ltd Bw. Gilbert Herman wakati wa hafla fupi ya kusainiana mkataba huo iliyofanyika Utumishi jana. Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Serikali Mtandao (eGA) Dkt.Kuwe Bakari. 

Katibu Mkuu Utumishi Bw. George D. Yambesi (katikati) akizungumza wakati wa hafla fupi ya kusaini mkataba wa kuweka Mtandao wa Mawasiliano wa Serikali  na kampuni za mawasiliano za SOFTNET Technologies na TTCL iliyofanyika jana Ofisini kwake. Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Serikali ya Serikali Mtandao (eGA) Dkt Kuwe Bakari, kushoto ni Bw. Priscus Kiwango Mkurugenzi wa TEHAMA Utumishi, akifuatiwa na Mkurugenzi wa kampuni ya SOFTNET Ltd  Bw.Gilbert Herman 

Baadhi ya wajumbe walioshiriki hafla fupi ya kusaini mkataba wa kuweka Mtandao wa Mawasiliano wa Serikali  na kampuni za mawasiliano za SOFTNET Technologies na TTCL iliyofanyika jana Ofisini kwake.

Monday 14 April 2014

TBS KUINUA WAJASIRIAMALI WADOGO NCHINI

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini kutoka Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi. Vedastina Justinian akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu Mradi wa Vituo vya Utoaji Huduma kwa Pamoja Mipakani (One Stop Border Posts) unaolenga kurahisisha taratibu za forodha, uhamiaji, usimamizi wa ubora wa bidhaa, ulinzi na usalama. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Miundombinu ya Kiuchumi Mhandisi Abdillah Mataka na kulia ni Afisa Habari wa Idara ya Habari Maelezo Bw. Frank Mvungi.

Mkurugenzi Msaidizi Miundombinu ya Kiuchumi kutoka Wizara ya  Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhandisi Abdillah Mataka, akifafanua kwa waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu ushiriki wa nchi wanachama wa Jumuiya hiyo katika kujenga vituo vya utoaji huduma mipakani kwa kila nchi husika ili kurahisisha shughuli za utoaji huduma za forodha na uhamiaji. Ujenzi wa vituo hivyo hapa nchini unafadhiliwa na Benki ya Dunia na Shirika la Maendeleo ya Japan. Kushoto ni Mchumi Idara ya Biashara na Sekta za Uzalishaji kutoka wizara hiyo Bw. Amedeus Mzee.

Mchumi Idara ya Biashara na Sekta za Uzalishaji kutoka Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Amedeus Mzee akizungumzia faida zitakazopatikana kwenye mradi wa vituo vya utoaji huduma kwa pamoja mipakani, aidha alitoa wito kwa wananchi kushirikiana na watumishi wa vituo hivyo katika kuhakikisha mapato hayapotei kwa maslahi ya nchi yetu na jumuiya kwa ujumla.

SERIKALI KUKAMILISHA VITUO VYA UTOAJI HUDUMA MIPAKANI

WIZARA YA  USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI
Na Frank Mvungi-Maelezo

Serikali imejipanga kukamilisha vituo vya utoaji wa huduma kwa pamoja Mipakani (One Stop Border Posts-OSBP) vitakavyosaidia kurahisisha taratibu za forodha,uhamiaji,Usimamizi wa ubora wa bidhaa na huduma ,usalama na ulinzi kwa kutoa huduma hizi upande mmoja wa mpaka.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Vedastinian Jastinian wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam.

Akieleza faida za vituo hivyo, Vedastinian amesema vitaondoa urasimu uliokuwepo awali na kuharakisha huduma na kwa wananchi wa nchi wanachama wakati wanapotaka kusafirisha bidhaa kutoka nchi moja kwenda nyingine.

Alisema Kituo cha kwanza ni kile cha Holili ambacho kimekamilika na kimekabidhiwa  kwa mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) ambao ndio waendeshaji wa vituo hivyo hapa nchini ambapo mradi huu unatarajiwa kukamilika mwezi Mei 2014.
Alifafanua kuwa katika mipaka ya Sirari/Isebania unazitenganisha Tanzania na Kenya na kwa upande wa Mkoa wa Mara mpaka wa Mutukula unazitanganisha Tanzania na Uganda.

Vedastinian alivitaja vituo vingine kuwa ni Namanga cha Arusha,Kabanga/Kobero kilichopo mpakani mwa Tanzania na Burundi unatarajiwa kukamilika mapema mwezi novemba 2014.

Alitaja vituo vingine ni Horohoro Mkoani Tanga na Lungalunga upande wa nchi ya Kenya ambapo ujenzi wake unatarajia kukamilika mapema mwaka huu.
Mradi huo unatekelezwa baada ya kutungwa sheria ya jumuiya ya Afrika Mashariki ya kuanzisha vituo vya utoaji wa huduma kwa pamoja mipakani (OSBP) Katika nchi wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki.

Sheria iliyopitishwa na Bunge la Afrika Mashariki na Iko katika hatua za mwisho za kuidhinishwa na Wakuu wan chi wanachama.


WATUMISHI WA UMMA WAFANYA BONANZA LA MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA MUUNGANO





Baadhi ya watumishi wa Umma kutoka Taasisi mbalimbali za Serikali wakifanya mazoezi mepesi wakati wa Bonanza la Maadhimisho ya Miaka 50 ya Muungano lililofanyika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Thursday 10 April 2014

UTUMISHI YAFANYA KIKAO KAZI KWA VIDEO CONFERENCE KATI YAKE NA MIKOA YA TANGA,DAR ES SALAAM,MOROGORO NA MWANZA

Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma  Bw. Hassan Kitenge (kulia) akiwasilisha mada kwa njia ya kielektroniki (video conference) katika kikao kazi  kati ya Utumishi na Mikoa ya Tanga,Dar es Salaam,Morogoro na Mwanza kilichofanyika ukumbi wa Utumishi mapema leo.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. George D. Yambesi akifuatilia mada wakati wa kikao kazi kilichofanyika kwa njia ya kielektroniki (video conference) kati ya Utumishi na Mikoa ya Dar es Salaam,Tanga,Morogoro na Mwanza katika ukumbi wa Utumishi  mapema leo. Kulia ni Mkurugenzi wa TEHAMA Bw.Priscus Kiwango akifuatilia mada.

Wednesday 9 April 2014

AMERICAN BILLIONAIRE HOWARD BUFFETT IN SERENGETI AND NGORONGORO


The American Billionaire Howard Buffett is visiting Serengeti National Park and Ngorongoro Crater for a three days holiday after he was very much impressed by Tanzanian tourist attractions when he visited the country last month.
During his last visit in the country in March this year, Howard Buffett, who has a passion on conservation matters through his Howard Buffett Foundation. donated two helicopters to Tanzanian Government to be used for anti-poaching activities in the protected areas.
At the Kilimanjaro International Airport, Buffett ,who is accompanied by his wife, was received by his host the Minister for Natural Resources and Tourism Hon. Lazaro Nyalandu.


Howard Buffett received by his host Minister for Natural Resources and Tourism Hon. Lazaro Nyalandu

Howard Buffett coming out of his private jet at Kilimanjaro International Airport.

Howard Buffett dances with the Maasai Cultural Group at KIA. 

Ghoosh….i can also jump high like a Maasai…Buffett seems to say so..

Let us see who can jump high…

Howard Buffett dances with the Maasai women.

Minister for Natural Resources and Tourism Hon. Lazaro Nyalandu presents a grant gazelle trophy to Howard Buffett at KIA.

Add caption


Source ; TANAPA website

Tuesday 8 April 2014

MWAKILISHI JIMBO LA KIEMBE SAMAKI ATIMIZA AHADI KWA TIMU ZA JIMBO LAKE

Mwakilishi wa Jimbo la Kiembe samaki Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (wakatikati) wakiteta jambo na Mwenyekiti wa CCM Jimbo la Kiembe samaki Ramadhan Mrisho wa kushoto, kulia Mwenyekiti wa Kamati ya michezo ya Jimbo hilo Juma Abdul-rabi kabla ya kukabidhi pesa taslim na vifaa vya michezo kwa tim za Jimbo hilo ikiwa ni ahadi aliyoitoa wakati wa kampeni zake hafla hiyo imefanyika katika Hoteli ya Ocean View Mjini Zanzibar.

Diwani wa Jimbo la Kiembe samaki Bw. Gharib Mohamed Addy akizungumza na wanamichezo wa Jimbo hilo (hawapo pichani)kabla yakukabidhiwa vifaa vya michezo na Mwakilishi wa Jimbo la Kiembe samaki Mhe. Mahmoud Thabit Kombo

Baadhi ya wanamichezo na viongozi mbalimbali wa Jimbo la Kiembe samaki wakimsikiliza Mwakilishi wa Jimbo hilo Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (hayupo pichani) kabla ya kukabidhi pesa na vifaa vya michezo kwa timu za Jimbo lake. 
Mhe. Mahmoud Thabit Kombo akimkabidhi pesa sh/= laki nne kiongozi wa tim ya Smoll Zico ya Kiembe samaki ikiwa ni ahadi aliyoito wakati wa kampeni zake.

(Picha na  Makame Mshenga,MAELEZO ZANZIBAR)

TANZANIA WINS STREET CHILD WORLD CUP IN BRAZIL




The finals of the 2014 Street Child World Cup took place in Rio de Janeiro on Sunday. In the boys competition, Burundi managed to secure the cup with an impressive 3-1 win over Tanzania, while the hosts Brazil beat the Philippines 1-0 in the all-girls final. The 2014 Street Child World Cup, an initiative of Street Child United, a UK based charity, united teams of children from 20 countries.

Source:RT

Friday 4 April 2014

TUME YAANZA UTAFITI KATIKA MAPITIO YA MFUMO WA SHERIA UNAOSIMAMIA HAKI ZA WALAJI

Katibu Msaidizi wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Bw. Adam Mambi akiwaeleza waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu Mpango wa kuanza utafiti katika mapitio ya mfumo wa sheria unaosimamia haki za walaji ikiwa ni hatua mojawapo katika mchakato wa kuundaa  sheria inayowalinda watumiaji wa huduma mbalimbali hapa nchini. Kulia ni Afisa Sheria wa Tume hiyo ni Fred Kandonga.

Afisa Sheria wa wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Fred Kandonga akijibu maswali ya waandishi wa habari kuhusu sababu zilizopelekea Serikali kuamua kufanya utafiti utakaopelekea kutungwa kwa sheria itakayosaidia kuwepo kwa mfumo nwa biashara wenye uwiano katika ushindani. Katikati ni Katibu Msaidizi wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Bw. Adam Mambi, anayemfuatia ni Afisa Habari Idara ya Habari Maelezo Frank Mvungi na Mwisho kushoto ni Afisa habari wa Tume hiyo Munir Shemweta.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
TUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA

Anuani ya simu: "TUMESHERIA”.                                                                                P.O.Box 3580      
Simu ya mdomo; 2111387/2123533/4                                                                      DAR ES SALAAM
Namba ya fax: 2123534                                                                                                                                              
Barua pepe: lrct@lrct.go.tz
                                                                  
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
TUME YAANZA UTAFITI KATIKA MAPITIO YA MFUMO WA SHERIA UNAOSIMAMIA HAKI ZA WALAJI

Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania imeanza kufanya utafiti wa  mfumo wa sheria unaosimamia Haki  za Walaji ili kubaini kasoro mbalimbali zilizoko kwenye  mfumo husika na kupendekeza njia sahihi ya kuboresha mfumo huo nchini Tanzania.

Hatua ya Tume kufanya utafiti huo inatokana na mendeleo ya sayansi, teknolojia pamoja na utandawazi ambayo kwa ujumla yamemfanya mlaji kujikuta akiwa kwenye hatari ya kuathirika kiafya, kiuchumi na kijamii.

Tume katika utafiti wa awali, imebaini kuwa Mfumo uliopo hauendani na  na wakati huu wa mabadiliko ya kiuchumi, kijsamii, kitekenologia yanayotokea, kwani sheria nyingi zilizopo zilitungwa muda mrefu na hivyo hazikuzingatia mahitaji ya wakati wa sasa.

Pia sheria nyingi  hazijajumuishwa kwenye sheria moja  zinasimamiwa na watu au Taasisi tofauti tofauti. Hivyo, Tume imeona haja ya kupitia sheria hizo ili kupendekeza  mfumo wa sheria utakaomlinda mlaji kwa kuzingatia maendeleo yaliyopo sasa.
Na ni matarajio yetu baada ya kukamilika kwa utafiti huu Tume tutakuja na mapendekezo ambayo yataleta tija kwa walaji wetu pamoja na taifa kwa ujumla.
Tume ya Kurekebisha Sheria (Tume) ilianzishwa chini ya kifungu cha 3 cha Sheria ya Kurekebisha Sheria Namba 11 ya mwaka 1980. Sheria hii kwa sasa ni Sura ya 171 ya Sheria za Tanzania Toleo la Mwaka 2002. Tume ya Kurekebisha Sheria ni Idara ya Serikali inayojitegemea chini ya Wizara ya Katiba  na Sheria. 

Imetolewa na;
Tume ya Kurekebisha Sheria (T)
Dar es Salaam
04 Aprili, 2014


BIG RESULTS NOW' KUFANIKISHA UBIA KATI YA SEKTA BINAFSI NA ZA UMMA

Msemaji Mkuu wa Wizara ya Fedha, Ingiahedi Mduma, akizungumza wakati wa Semina maalum kwa 'Mablogger', iliyofanyika katika Hoteli ya Kilimanjaro Park, Misugusugu Kibaha, hivi karibuni. Semina hiyo imeandaliwa na Wizara ya Fedha kwa lengo la utaratibu wa kutimiza utekelezaji wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now). Picha na Sufianimafoto.com

Thursday 3 April 2014

TFDA YATOA MATOKEO YA UKAGUZI MAALUM WA MADUKA YA BIDHAA ZA VYAKULA JIJINI DAR, YAWATAKA WANANCHI KUJENGA UTARATIBU WA KUSOMA MAELEZO YA BIDHAA KABLA YA KUNUNUA.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA) Bw.Hiiti Sillo akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu ukaguzi maalum wa maduka ya kuuzia vyakula   “Supermarkets”
 na Mini-Supermarkets  katika jiji la Dar es salaam.

 Mkurugenzi wa Usalama na Chakula wa TFDA Bw. Raymond  Wigenge akitoa ufafanuzi kwa waandishi kuhusu hatua zinazochukuliwa na TFDA kuhakikisha usalama wa vyakula na Dawa nchini .TFDA imekuwa ikiongeza nguvu katika kukabiliana na bidhaa zisizokidhi viwango kwa kushirikiana na mamlaka nyingine za udhibiti kwa kukagua, kukamata na kuchukua hatua za kisheria ikiwemo kuwafikisha wanaokiuka sheria.

 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA) Bw.Hiiti Sillo (kulia) akitoa ufafanuzi wa baadhi ya bidhaa zilizokamatwa katika ukaguzi maalum kwenye maduka ya kuuzia vyakula   “Supermarkets” na Mini-Supermarkets  katika jiji la Dar es salaam zikiuzwa kinyume cha sheria ya Chakula , Dawa na Vipodozi sura ya 219. Wengine ni Mkurugenzi wa Usalama naChakula wa TFDA Bw. Raymond  Wigenge,na Meneja wa Ukaguzi wa Chakula wa TFDA kanda ya Mashariki Bw. Emmanuel Alphonce.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA) Bw.Hiiti Sillo (kulia) akitoa ufafanuzi wa maziwa yaliyokamatwa yakiwa kwenye kifungashio kisichokua na maelezo yoyote yakiuzwa kwenye maduka ya kuuzia vyakula   “Supermarkets”na Mini-Supermarkets  katika jiji laDar es salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA) Bw.Hiiti Sillo (kulia) akitoa ufafanuzi wa baadhi ya bidhaa zilizokamatwa katika ukaguzi maalum kwenye maduka ya kuuzia vyakula   “Supermarkets” na Mini-Supermarkets  katika  jiji la Dar es salaam zikiuzwa kinyume cha sheria ya Chakula , Dawa na Vipodozi sura ya 219. Wengine ni Mkurugenzi wa Usalama na Chakula wa TFDA Bw.Raymond  Wigenge, na Meneja wa Ukaguzi wa Chakula wa TFDA kanda ya Mashariki Bw. Emmanuel Alphonce.

 Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA)Bi. Gaudensia Simwanza akiwaonesha waandishi wa habari baadhi ya bidhaa zilizokamatwa na mamlaka hiyo  zikiwemo chumvi, vinywaji, maziwa ya watoto ambazo hazijasajiliwa na mamlaka hiyo kufuatia ukaguzi maalum uliofanyika katika jiji la Dar es salaam.

 Maziwaya watoto aina ya SMA 1,2 na 3, Promil Gold, S-26 Gold, Nursoy, Progress Gold, Cow &Gate, Isomil 2 na Infacare Soya , Nutrikids na Aptimil 1 yaliyokamatwa ambayo hayajasajiliwa na TFDA .


 Vinywaji baridi ambavyo havikusajiliwa na TFDA vilivyokamatwa kufuatia ukaguzi maalum katika jiji la Dar es salaam.Picha na 10.Bidhaa za chumvi ambazo hazikusajiliwa na TFDA zilizokamatwakufuatia ukaguzi maalum katika jiji la Dar es salaam.